Bolt atawala mita 100 Beijing
Bingwa wa dunia was
mbio za matimko za mita 100 kwa upande wa wanaume,Usain Bolt wa
Jamaica, amejifurukuta na kuwapiku wapinzani wake wakuu alipohifadhi
taji lake la dunia mbele ya umati mkubwa uliojitokeza kushuhudia fainali
hiyo katika uwanja wa kimataifa Birds Nest Beijing China.
Bolt alitoka nyuma na kuukata utepe katika fainali iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na ghamu na watu wengi zaidi katika mashindano ya riadha duniani yanayoendelea nchini China.
Raia wa Canada, Andre de Grasse na Mmarekani Trayvon Bromell walisajili muda wa sekunde 9.92 na kutuzwa medali ya shaba.
Bolt atakumbukwa kwa kuibuka kidedea kati8ka mbio za matimko alipozoa medali za dhahabu katika mbio za mita 100 na mita 200 katika mashindano ya olimpiki mwaka wa 2008 huko huko Beijing.
Comments
Post a Comment