Hii ya magereza 9 duniani kubadilishwa kuwa mahoteli makubwa imenifikia, Africa ipo moja tu!
Nimekutana na stori moja kwenye mitandao inayohusiana na magereza ya zamani ya wafungwa, yamekusanywa magereza 9
ya sehemu mbali mbali duniani na kubadilishwa kuwa kitu tofauti kabisa,
na ukiyaona hutoamini kuwa majengo hayo yalishawahi kuwa magereza ya wafungwa!
Kwenye yale maeneo ambayo Serikali waliacha kuyatumia kama maeneo ya magereza ya wafungwa yamechukuliwa na kubadilishwa kuwa hoteli au shule mtu wangu, majengo ni yale yale sema ubunifu mdogo tu umetumika kuyageuza majengo hayo kuwa sehemu ya vivutio kwa watalii.
Na kwa msaada
wa teknolojia ya kisasa kabisa sehemu hizi zimegeuzwa kuwa sehemu nzuri
sana, zenye mvuto na kama ukitembelea maeneo hayo bila kujua historia
ya sehemu hiyo itakuwa vigumu sana kwa wewe kujua kuwa jengo au eneo
hilo lilikuwa la wafungwa magereza.
Hapa chini
nimekusogezea picha 9 za maeneo na magereza mbali mbali duniani ambayo
kwa sasa zinaweka headlines tofauti na miongoni mwa picha hizi kuna moja
kutoka Lagos Nigeria iliyoweka headlines.
Hii ni Louviers Music School iliyopo Ufaransa lakini kabla ya mwaka 2011 jengo hili lilikuwa la wafungwa magereza.
Museum
of Belize ipo kaskazini mwa Marekani kwenye mji mdogo uitwao Belize
City, na kabla ya mwaka 2002 jengo hili lilitumika kuhifadhi wafungwa.
Cultural
Park of Valparasio ni hoteli iliyopo China na kabla ya mwaka 1999 jengo
hili lilitumika kama gereza la viongozi kwa kisiasa.
Hii
hoteli inaitwa Four Seasons Istanbul at Sultanahmet ipo Turkey mtu
wangu lakini napo palishawahi kuwa sehemu ya kuhifadhia wafungwa.
Pentridge
Prison ipo Australia lakini wenyewe hajabadilisha vitu vingi sana toka
mwaka 1999 ila ni miongoni mwa hoteli zinazolaza watu wengi sana.
Hostel Celica, wenyewe wanakupa ile mandhari halisi ya gerezani na palishawahi kuwa gereza la wanajeshi.
Comments
Post a Comment