FARID MUSSA SASA MAMBO SAFIIIIII NJIA NYEUPE KWENDA HISPANIA

Image result for picha faridi musa 

Wakati wasiwasi ukiwa umetanda kwamba huenda ndoto za Farid Musa kucheza soka la kulipwa Ulaya zikawa zimefifia, sasa kuna habari njema kwamba kiungo huyo mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania
‘Taifa Stars huenda akasafiri kwenda kujiunga na timu yake ya Tenerife inayoshiriki ligi daraja la kwanza nchini Hispania.
Awali suala la Farid kuendelea kuonekana Tanzania huku akiwa amefuzu majaribio kwenye klabu ya Tenerife lilizua mijadala hadi kupelekea nahodha wa timu ya taifa Mbwana Samatta kuhoji nini kimefichika nyuma ya pazia juu ya Farid kujiunga na timu yake ambapo tayari alishafuzu majaribio.
 Image result for picha faridi musa
General Manager wa Azam FC, Abdul Mohamed amethibitisha kukamilika kwa kibali ambacho kitamruhusu Farid kufanya kazi nchini Hispania na ameahidi kuwa, klabu inafanya jitihada kuhakikisha Farid anaondoka mapema kwenda kujiunga na klabu yake ya Tenerife.
“Kibali chake cha kazi kimetoka siku moja ama mbili zilizopita, sasahivi tunasubiri kukamilika kwa baadhi ya taratibu na punde Farid ataelekea nchini Hispania kwenye timu ya Tenerife kwa ajili ya kuanza maisha yake mapya,” amethibitisha Abdul Mohamed.
“ITC ya Farid imetumwa muda mrefu sana ipo Tenerife masuala ya ITC na makubaliano kati ya klabu na klabu tulishamaliza kilichokuwa kinasubiriwa ni kibali cha kazi kutoka ili kwenda kufanya kazi.”
“Tunaamini punde Farid ataanza safari yake, tunajitahidi hadi kufikia mwisho wa mwezi huu kila jambo liwe limekamilika.”
farid-musa-kibali



Comments

Popular Posts