HIGUAIN AISALITI NAPOLI APIGA BAO JUVENTUS IKISHINDA 2_1

 Image result for picha HIGUAIN
Gonzalo Higuain Jana alufunga Bao la ushindi kwa Juventus dhidi ya Klabu yake ya zamani Napoli kwenye Mechi ya Ligi Serie A huko Italy.

Bao hilo lilikuja Dakika ya 71 kwenye Mechi iliyochezwa huko Juventus Arena Jijini Turin na kuwapaisha Mabingwa Watetezi Juve kileleni mwa Serie A wakiwa Pointi 5 mbele ya Timu ya Pili AS Roma.
Juve sasa wana Pointi 27 kwa Mechi 11, AS Roma Pointi 22 kwa Mechi 10 na kufuatia Napoli wenye 20 kwa Mechi 11 na AC Milan ni wa 4 wakiwa na Pointi 19 kwa Mechi 10.
Jana Juve walitangulia kwa Bao la Dakika ya 50 la Leonardo Bonucci na Napoli kurudisha Dakika ya 54 kupitia Jose Callejon.
Lakini Shujaa akawa Higuain katika Dakika ya 71 kwa Shuti ambalo lilimzidi Kipa Pepe Reina.

Comments

Popular Posts