KAKWAYA100 BLOG INAKUPA MBINU ZA KUMTONGOZA MWANAMKE ULIE MPENDA

Kujifundisha jinsi ya kumuapproach mwanamke kwa mara ya kwanza si jambo gumu la kufanya kama utafuata kanuni na masharti na kuyahifadhi baadhi ya michongo kwa moyo. Michongo ni maneno ya kwanza ambayo mtu hutumia kuanzisha maongezi na mwanamke.

1. Matukio
Aina hii ya michongo ni rahisi kuikumbuka na ukiitumia kwa mwanamke atakupa atenshen yake automatic. Michongo hii hutumika ili kutaka atenshen ya mwanamke kwa kujaribu kumuuliza maswali ambayo yanalingana na mazingira aliyeko.
Baadhi ya aina ya michongo iliyofunge ni kama:
"Unaweza kujua wakati gani gari lingine la abiria linaweza kufika hapa?"

"Je unajua sehemu nzuri ambayo mtu anaweza kujiinjoy katika huu mji?"

"Nlikuwa nataka kuvuta sigara lakini kibiriti changu sikioni, naweza kuomba chako?"

"Nilikuwa sijamaliza kuandika maswali ya mwalimu kwa ubao, unaweza kunisaidia kitabu chako?"

2. Kumsifu
Aina hii ya michongo inakaribiana na ile ya wazi lakini kwa mpango flani inazuia kumfanya mwanamke kuelewa ajenda yako kwa uharaka. Michongo hii inafaa zaidi wakati ambapo inatumika katika vilabu, sehemu za kujivinjari ama sehemu yeyote ile ambayo unaona inaweza kutumika.
Kabla hujamsifu, ni lazima uhakikishe ni kwanini unamsifu manake mara nyingi unapomsifu mwanamke kuhusu jambo fulani atataka kujua kwa nini unammiminia sifa kama hizo.
Baadhi ya michongo ya kumsifu ni kama vile;

"Dress uliyoivaa imekupendeza, yaani imekufanya kuonekana mfano wa malaika"

"Una pozi lengine ajab, lazima wewe ni dansa flani"

"Nimependezwa na mtindo wako wa nguo na umbo lako, umetoklezea"

Ujanja wa kutumia aina hii ya michongo ni kuhakikisha unacheza na tabia na umbo lake, hakikisha kuwa unajaribu kumchunguza ili kupata mambo ambayo anayapenda kumhusu yeye. Usisahau ya kuwa utafiti umebainisha kuwa wanawake hupenda sana kusikia wakisifiwa.

3.  Kuangazia mazingira
Kulingana na mazingira, unahitaji kuifahamu sanaa ya kuingia katika akili ya mwanamke na kufahamu kile ambacho anafikiria. Ukifahamu kile ambacho anafikiria, itakuwa ni jambo jema zaidi.
Kwa mfano,  kama mwanamke anajaribu kusoma lakini kila dakika anasumbuliwa na jambo fulani, unaweza kumuuliza: "Si inaonekana ni vigumu zaidi kusoma wakati ambapo jua ni kali zaidi huko nje?"

Kama umekutana na kundi la wanawake na ungetaka kuanza kuongea nao, unaweza kuwaapproach halafu useme "Nyinyi wanawake mnaonekana mnaenjoy sana na wenye nishati, kwani kitu gani kinachoendelea ambacho nakikosa?"

Pia kama kuna mwanamke unayemzimia na hujawahi kuongea na yeye unaweza kumwambia "happy birthday"

Maneno ya kutumia Baadhi ya michongo iliyowazi ni kama vile:
"Unaoneka mrembo, unaweza kuniruhusu nitake kukujua zaidi?"

"Nilikuwa nimekuona kutoka upande ule mwingine wa nyumba na nikaamua kuja kukusalimia, bila hivyo ningeishi kujutia kukosa kumjua mwanamke mrembo zaidi maishani mwangu"

Mwisho ni kuwa hakikisha kuwa baada ya kutumia hii michongo kupata atenshen ya mwanamke, hakikisha unaendeleza maongezi yenu. Jaribu kupata kulijua jina lake halafu ujibidiishe kulitumia kila wakati, lazima atapenda.

Usisahau kutumia sanaa za kutongoza kwa kujua vitu ambavyo mnagawa interest pamoja, jinsi ya kumfurahisha na kadhalika. Hii utamfanya apendezwe na wewe na mudan usiomrefunatakuzoea.

Comments

Popular Posts