MAKALA ATAKA WALA RUSHWA WAFICHULIWE





Mkuu Wa Mkoa Wa Mbeya Amos Gabriel Makala

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amosi Gabriel Makalla amewataka wananchi kusaidia katika kujenga maadili ya watumishi wa umma kwa kufichua vitendo vya ukiukwaji wa wa utumishi wa umma ikiwemo rushwa.
Ameyasema hayo kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya maadili ambapo pia amewataka watumishi wa umma kupiga vita rushwa na ukiukwaji wa haki za binadamu kwa vitendo.
Ameongeza kwa kusema kuwa serikali kwa kuzingatia maadili imetekeleza mipango mikakati mbalimbali ya kitaifa na kimataifa ya kupambana na rushwa ikiwa ni pamoja na kuanzisha mkakati wa kukuza uchumi na kuondoa umasikini Tanzania MKUKUTA na kuanzisha siku ya maadili duniani ni ishara tosha ya kuonesha wamechukua hatua.
Aidha amesema vita dhidi ya rushwa na madili ni ya kila mmoja sio kuziachia tu mamlaka zinazohusika pekee kwa kuwa kwa kufanya hivyo ni ngumu kupambana na rushwa na kuimaliza kabisa.
Naye mkaguzi wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU wa kanda ya kusini Joyce Shundi akitoa shukrani kwa mgeni rasmi amesema watafanyia kazi hotuba ya mkuu wa mkoa kwa kutoa huduma yenye tija kwa jamii.
Amesema wiki nzima hii ya maadili wametoa elimu kupitia vituo vya redio mkoani Mbeya, kwenye shule, vyuo na taasisi za dini huku wakifanya usafi katika hospitali ya Igawilo.
Maadhimisho ya siku ya maadili kwa mkoa wa Mbeya yamefanyika katika viwanja vya ofisi ya TAKUKURU mkoa wa Mbeya huku yakichagizwa na kauli mbiu inayosema kujenga na kukuza maadili, haki za binadamu, uwajibikaji, utawala bora na mapambano dhidi ya rushwa.


Comments

Popular Posts