Vipodozi haramu, vyakula vyenye sumu vyakamatwa Songea

Endelea kutembelea blog yetu kuwa wa kwanza kuhabarika kwa maoni na ushauri +255 766 086 039 +255 625 715 167 +255 744 063 802 +255 719 980 891 +255 684 219 786



Idara ya Afya katika Manispaa ya Songea imefanikiwa kukamata vipodozi na vyakula vyenye sumu vikiwa na thamani ya zaidi sh.milioni mbili.

Afisa Habari wa Manispaa hiyo Albano Midelo amesema vipodozi hivyo vimekamatwa katika kipindi cha kuanzia Aprili hadi Juni mwaka huu katika ukaguzi endelevu ambao unafanywa na Idara hiyo.
Amevitaja baadhi ya vipodozi vyenye sumu ambavyo vimekamatwa kuwa ni actif plus, betasol, broze, cocoderm, carolight, carotone, citrolight,clairmen,cocopulp,corton,diproson na epiderm.
Vipodozi vingine ni,extralair,jaribu,lemonvate na mekako, miki, Montclair, movate, Naomi, oranvategel, perfect, princes, rapid, sabuni protex,seven mirackes, toplemon, whiteplus, dodo, teint, superclair,greeting,14 days, dermotyl, natural,gold touch,coco dermbetacort,extral white, fomura avas, lemon cream na diva maxmum.
Midelo amesema katika ukaguzi huo pia vimenaswa vipodozi halali ambavyo vimemalizika muda wake vyenye thamani ya zaidi ya sh.500,000.Vipodozi vilivyomalizika muda wake ni skin soft,pure glycerine,royal touch,u&me na mambo fresh.
Katika kipindi hicho Idara hiyo pia imekamata vyakula vilivyokuwa vinauzwa wakati muda wake umekwisha vyenye thamani ya zaidi ya sh.300,000.

Comments

Popular Posts